Swahili

Kusakamwa ama kutokanywa?


Ukinibusu sitakufikiria tena
Ukinidharau kwako sitanena
Nisipomaliza kazi utafanya?
Hii kalamu nimeshikilia sijasanya.
Nikikimbia najikwaa
Nikitembea nachelewa
Nifikapo kwako napigwa na butwaa
Maneno yangu wakataa kuyaelewa
Uwe mwalimu ama mpenzi wangu
Kilicho muhimu ni kwamba maisha ni yangu

Maisha ni yako?
Nani kakudanganya?
Mwili si wako hata matako.
Salala matakwa nimejikanganya.
Ukiwa wewe kisiwa basi maji ni nani?
Bila ziwa wewe ni mlima pweke
Sitaki kukusukuma maishani
Lakini mawaidha yangu uyaweke.
Nikikuzaba kofi usilie.
Kabla uchome nyumba yangu,si ufikirie?

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s